Wednesday 25 May 2011

MWISHO WA DUNIA ULITABIRIWA 21-05-2011







Mhubiri wa dini bwana Harold Camping mwenye umri wa miaka 89 kutoka Oaklnd,Califonia ,alitabiri mwisho wa dunia.Mhubiri huyu alitangaza kupitia "Familly Radio"ambayo inarusha matangazo na kuhubiri dini ya kikristu.Alitabiri mwisho huu ni siku ya jumamosi tarehe 21-05-2011 na akasema ya kwamba asilimia mbili (2%) wataingia peponi na watakaobaki watapelekwa sehemu tofauti.Lakini kiliwashangaza wengi kwa wale waliosikiliza habari hiyo kupitia Familly Radio kutoona mwisho huo aliouzungumzia na kuwapa watu mshangao na kujiuliza maswali mengi.Na amesikika katika televisheni akiomba radhi watu kwa kutotabiri kwa usahihi.Sasa tusubiri utabiri ujao kama kweli sisi binadamu tunanguvu ya kujua mambo aliyoyapanga mwenyezi mungu,na yana siri kubwa na hakuna atakayekuwa na uwezo wa kujua siri hiyo.

No comments:

Post a Comment